MWISHO WA UBAYA AIBU


mwisho wa ubaya aibu



na
aziza a. zaburi


SHUKRANI
 Kwanza, napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu (Allah(s.w)) muumba na muweza wa kila kitu, kwa kunijaalia afya njema, nguvu, uwezo, akili, busara, maarifa, utulivu na uvumilivu katika kipindi chote cha masomo yangu. Namshukuru tena kwa unyenyekevu pamoja na tauhidi kwa kusema, Alhamdulillah Rabbil 'alamin.
Pili, napenda kumshukuru kwa dhati kabisa, mwalimu wangu wa somo la Kiswahili kwa kuniongoza vyema katika kila hatua kuandika kitabu hiki. Hakusita wala hakuchoka kunishauri na kunirekebisha namna ya kuandika vitabu ikapelekea kukamilisha kuandika kitabu hiki. Amenilea kitaaluma pamoja na kunifunza misingi ya nadharia za fasihi, fasihi fafanuzi na mbinu za uandishi wa vitabu ambazo zimezaa kazi hii. Namuomba Mwenyezi Mungu ambariki na ampe afya njema pamoja na ukakamavu na amzidishie kila la kheri, na kumuepusha na kila la shari, Amin.
Tatu, napenda kuishukuru familia yangu kwa uvumilivu waliouonyesha kwa kuelewa kuwa nilikuwa nafanya kazi ya shule, kwani kwa baadhi ya nyakati walikosa kunitumia katika kazi mbalimbali za nyumbani wakanipa muda ili nikamilishe kazi hii.
Nne, napenda kuwashukuru walimu wangu wa shule ya sekondari Engusero kwa kunilea kitaaluma na kunikuza kinadharia na vitendo. Walimu hao ni pamoja na Mkuu wa shule, Makamu mkuu wa shule, Mtaaluma na waalimu wengine wote wa shule ya sekondari Engusero.


TABARUKU
Natabaruku kazi hii kwa wazazi wangu, Bw. Athumani Zaburi na Bibi Amina Omari kwa kunizaa, kunilea, kunisomesha, kunifunza mema, kunikataza mabaya, na kunipa moyo na kuniwezesha kifkira na maadili mema katika kipindi chote cha masomo yangu, tangu darasa la kwanza mpaka sasa kidato cha sita. Mawazo yao na busara zao katika elimu nitazikumbuka daima na kuwa chachu ya kujiendeleza zaidi.
Vilevile ninawatabarukia kaka zangu Bashumu Athumani na Shiraji Athumani, kwa ushawishi, uvumilivu, huruma na kunitia moyo pale nilipokata tamaa katika masomo yangu mpaka leo nafikia kidato cha sita. Pia kwa msaada wa hali na mali katika kukamilisha kazi yangu hii, ikiwa ni pamoja na gharama za masomo na kuwa wasimamizi na nguzo imara na thabiti katika kuhakikisha sikati tamaa ila ninamaliza masomo yangu, tangu kidato cha nne mpaka leo kidato cha sita

KAZI HII INAPATIKANA PIA KATIKA TOVUTI IFUATAYO

 NENO LA WALI
Shukurani zote njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu (Allah (s.w)) aliye Bwana na Mlezi wa walimwengu wote.
Ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwafikisha kutoa kitabu hiki MWISHO WA UBAYA AIBU kama muendelezo wa kazi za kitaaluma katika somo la Kiswahili baada ya kutoa kitabu cha kwanza UZAZI WA MSOTO.
Lengo la kitabu hiki ni kuelimisha jamii juu ya matatizo wanayoyapata watoto yatima na wajane (wanawake waliofiwa na waume zao) kama vile:-
(i)                 Mke na watoto kufukuzwa katika majumba wanayoishi na Ndugu wa marehemu
(ii)               Watoto kukatisha masomo
(iii)             Kufanyiwa vitendo vya kikatili kama vile kubakwa na unyanyasaji wa kijinsia
(iv)             Kuzuka kwa ajira za utotoni
Wito wa mwandishi kwa jamii nzima, ni kuwatunza mayatima na wajane ni jukumu la jamii nzima kwani na yeye alikua na wazazi kama wewe naye alikua na mume kama wewe mwanamke uliye na mume.
SEHEMU YA KWANZA
            Tina alikuwa amelala kifudifudi kitandani pake akilia kwa majuto na upweke alioachiwa na mume wake kipenzi bwana Alfan. Zaidi ni yule mtoto aliyeachwa na baba yake yungali mdogo kila alipomwangalia mtoto wake huzuni na majonzi yalimtanda kwenye akili yake lile tumaini lote alilokuwa nalo lilitoweka ghafla Tina aliurejea upweke wake ambao aliachiwa na wazazi wake pale tu mume wake alipoaga dunia kwani mume wake alikuwa ni tegemezi lake la mwisho baada ya wazazi wake kupoteza maisha kwa ajali ya moto bwana alfani alikuwa ni msaada mkubwa kwa Tina alimpenda na alimthamin na kumpa heshima ya hali ya juu, bwana Alfani alikuwa na sifa za kipekee ambazo wanaume wengi wa kijiji chao hawakuwanazo, Tina alijivunia sana mume wake, lakini furaha yote ilipotea pale tu bwana Alfani alipoaga dunia Tina alijihisi ni mgeni wakati yupo kwenye nyumba yake alipambana na maswali magumu ambayo aliulizwa na mtoto wake aliyeitwa Chiku mara kwa mara, Chiku alikuwa ni mtoto mwenye umri wa miaka sita alipedwa sana na marehemu baba yake, alikuwa ni mtoto wa Darasa la kwanza kila alipo kwenda shule baba yake alimsindikiza kwa baiskeli huku akimsimulia hadith ambazo kila mtoto alizipenda, bwana Alfani alikuwa na upendo wa dhat kwa familia yake ambao ulimvutia kila mwanamke.
            Siku moja Tina na mwanawe walikuwa wameketi kwenye mkeka, huku akimsimulia hadithi ambazo alikuwa akisimuliwa na baba yake, lakini Chiku alionekana kuto kuwa na furaha, alimuuliza mama yake, mama baba yuko wapi? Tina alionesha kuto kumzingatia Chiku, Chiku alimuuliza tena mama yake, mama! Baba Yuko wapi? Tina akamwambia Chiku, mwanangu baba ameenda mjini atarudi kesho, hapana mama! Baba hatorudi kwa sababu watu wanasema baba amekufa! Chiku aliongea huku anabubujikwa na machozi Tina hakuelewa nini cha kumjibu mototo wake, alitokwa na machozi kisha akasema , mwanangu Chiku hao ni waongo, waongo? Hapana mama ni kweli, sasa nani atakaenipeleka shule? Nani atakae nisimulia hadithi za sungura na fisi? Mama niambie basi! Niambie mama yangu, Tina alimkumbatia mwanawe kisha akasema, mwanangu niamini mimi mama yako, wakati Tina anamliwaza Chiku, mlango uligongwa, ngo! ngo! ngo! Tina na Chiku walishtuka, mlango uligogwa tena, ngo! ngo! ngo!, Tina alinyanyuka akaenda Kufungua mlango alipofungua mlango, alikalibishwa na sura za watu wawili zimekunja kama sura za vikongwe, ilhali wao ni vijana, Tina aliwakaribisha kwa furaha, lakini cha ajabu wageni wale hawakujibu chochote wakaingia ndani wakaketi kwenye viti Chiku alielekea kule waliko wageni kisha akawasalimia, shikamoo baba mdogo, shikamoo baba mkubwa, wawili wale waliangaliana kisha wakaitikia kwa pamoja marahaba, Chiku aliendelea kwa kusema, eti baba anarudi lini? Baba yako?, Mmoja kati ya wawili wale aliyejulikana kwa jina la Kangomba alishangaa! Mwingine akaropoka Kwa kusema baba yako amekufa, Tina alidakia kwa kusema shemeji nini unamwambia mtoto? Hujui Kama……………………, Chiku aliangua kilio akamwambia mama yake, mama kumbe ni kweli baba amekufa? Tina alichukizwa na kitendo walichokifanya shemeji zake, lakini hakuwaonesha ni jinsi gani amechukia, akamnyanyanyua chiku kisha akasema mmewaacha wazima wote huko nyumbani? Kangomba akajibu, hatuhitaji salamu wala maongezi na wewe, ila tumekuja kwa ajili ya jambo moja tu, Kama bwana Alfani amesha kufa sasa unasubili nini kwenye nyumba hii, Jua kabisa kwamba hii nyumba si yako wala si ya alfani, tunaomba uchukue kilicho chako uondoke. Tina alihamaki kisha akasema siondoki nitabakia hapahapa, mnaponiambia niondoke na huyu mtoto ataishije? Na mimi nitaenda wapi? Utaenda wapi, Kabla haujaolewa na alfani ulikuwa unaishi wap? Mwingine kati ya wawili wale akasema kwa hiyo ulimroga Ndugu yetu ili urithi nyumba? Tina alilia huku anasema mbona hamna huruma hata kwa mtoto ambae ni damu ya Ndugu yenu? Tena nyamaza! Kangomba alipayuka tunavyo fahamu sisi Ndugu yetu hakuwa na uwezo wa kupata mtoto! Mh! Tina alipigwa na butwaa akasema kama Ndugu yenu hakukuwa na uwezo wa kupata mtoto sasa huyu mtoto ni wanani? Kwani nani asiye fahamu hapa kijijini kama wewe ni kahaba, Malaya, mzinzi, nani asiyejua si nakuuliza? usitucheleweshee muda wetu chukua kilicho chako ondoka, Kangomba aliingia chumbani  akakusanya mabegi ya Tina akayarusha nje akamzoazoa Tina na mwanawe chiku akawasukumiza nje, Tina alimuangalia mtoto wake akalia kwa uchungu na Chiku nae alipomuona mama yake analia na yeye akaanza kulia, Tina alipiga moyo konde akanyanyua mabegi yake moja akaliweka kichwani linguine mkononi na Chiku akambeba mgongoni kisha akasema ama kweli DUNIA HADAA ULIMWENGU SHUJAA, leo hii mimi nafukuzwa kama mbwa, naambiwa nimemroga mume wangu, alilia sana lakini hakuna aliyemsikiliza, kangomba na kaka yake  walifunga mlango kisha hao wakaondoka, wakamuacha Tina amechoka haelewi wapi kwa kwenda,       baada   ya dakika kadhaa na Tina nae akaondoka                                                                                                                                                                                                                      
 SEHEMU YA PILI
Tina na mtoto wake Chiku wapo njiani, Tina haelewi aelekee wapi, hana wazazi wala walezi ambao wataweza kumsaidia lakini aliwaza akajisemea kimoyomoyo, mmh! Nikiondoka mbali na kijiji hichi mwanangu hatosoma sasa nifanyeje? Aah! Mungu wangu naomba unisaidie mimi sina kwa kwenda, wala kwa kukimbilia, lakini alifikiria akaona aende kwanza akamuone wmalimu mkuu wa shule ambayo Chiku anasoma labda atamsaidia kwa namna moja ama nyingine. Bila kupoteza muda alimshika Chiku mkono na begi lake moja kichwani jengine mgongoni moja kwa moja hadi shuleni, alipofika alikuta ofisi imefungwa. Chiku alimwuliza mama yake, mama! umekuja kuniombea ruhusa? Tina alimfaiji mwanawe kwa kusema ndio mwanangu, ila leo si juma pili? Chiku alimuuliza mama yake, Tina alivunjika moyo kisha akamwambia mtoto wake, Chiku tuondoke mwanangu ofisi ya mwalimu imefungwa. Mama mimi nimechoka kutembea, nabaki hapa hapa nenda kamwambie baba anifuate na baiskeli, mwanangu Chiku njoo nikubebe mgongoni alafu baba atatukuta njiani, Chiku alikataa kata kata kisha akamwambia mama yake, mimi sitaki kuondoka nabaki hapa hapa hadi baba aje. Wakati Tina anaendelea kumbembeleza mtoto wake, kuna mwalimu alikua anaishi karibu na shule aliyejulikana kwa jina la mwalimu Doka, alikua anatembelea maeneo ya shule lakini aliona kama kuna watu wameketi kwenye benchi lililopo mbele ya ofisi ya mwalimu mkuu, akaelekea kule kule walipokua wamekaa, alipofika pale alishangaa kumwona Chiku na mama yake wamekaa na wote wana huzuni wa hali ya juu. Mama chiku, vipi mbona upo hapa ilihali leo ni Juma pili na mbona una mabegi makubwa hivi unaenda wapi? Mwalimu doka aliuliza, Chiku alikua amepitiwa na usingizi palepale, mama Chiku alimjibu mwalimu kwa upole, Ah! Mwalimu nahitaji ruhusa kidogo ya mwanangu hatohudhuria shule kwa siku kadhaa mambo yakikaa vizuri atahudhuria kama kawaida, mwalimu Doka alimuuliza unakwenda wapi? Tina alimjibu, sina kwa kwenda kaka yangu, natafuta nyumba nipange, alafu nitafute kazi ambayo itaniingizia fedha ili niweze kupata fedha ya kumlipa mwenyenyumba, Doka alishangaa akamuuliza tena unataka kupanga? Kwani nyumba uliyokua unaishi na marehemu mume wako haikua yakwenu? Tina aliangusha kilio mithili ya mtoto mchanga mwenye njaa, Mwalimu Doka akajitahidi kumnyamazisha Tina, kisha akamwinua akamwambia twende nyumbani kwangu ukapumzike kwanza Mwalimu Doka alimnyanyua Chiku akamweka begani kwake akabeba begi moja la nguo na jingine akalibeba Tina wakaelekea nyumbani kwa mwalimu Yule, walipofika mke wake aliwakaribisha wakaingia ndani, mwalimu Doka alimwamuru mkewe amchukue Chiku akamlaze chumabni, akamkaribisha Tina, nae akaketi kwenye kochi lililotandikwa kwa vitambaa vizuri vyenye rangi nyekundu yenye kumelemeta, mke wa mwalimu Doka alimkaribisha mama Chiku  kwa glasi ya juisi ya matunda. Kisha akamwambia jisikie upo nyumbani, kisha akamuomba mumewe waingie chumbani mara moja, walipofika tu! Mwalimu Doka alishangaa kumuona mke wake amevimba kama boko aliyeshiba maji ya mto, akamuuliza kuna shida gani? Mbona si kawaida yako kuwa hivyo? Mume wangu niambie yule mwanamke ni nani yako? Bite alimuuliza mune wake,kabla mumewe hajajibu akaendelea kwa kusema, mume wangu ujue mimi nakupenda sana sihitaji nikupoteze, hata mimi nakupenda mke wangu na sihitaji kukupoteza, na kuhusu Yule mwanamke usiwe na shaka kabisa, kuwa na amani ndani ya moyo wako mwalimu Doka alimwambia mkewe. Bite alinyanyuka akamkumbatia mume wake kisha akamwambia wasiwasi ndio akili na ni lazima niwe na wivu juu yako kwa sababu nakupenda saana, mwalimu Doka alitabasamu kisha akamwambia, kumbe nawe unawivu kiasi hicho? Usiwe na wasiwasi mimi ni wako daima, Bite alifurahi kwa maneno mazuri aliyopewa na mumewe, baada ya muda mchache Bite aliandaa chakula kwa ajili ya wageni na muda ule ule Chiku nae akaamka alishangaa kuona yupo peke yake kitandani  akaita kwa sauti kali mamaaa! Bite aliwahi chumbani akamnyanyua Chiku akamwambia usilie mtoto mzuri twende kwa mama, Tina alifurahi kumuona bite alivyokuwa na upendo na ukarimu usio na kifani, mwalimu Doka nae alifurahi kuona mke wake anawajali wageni, Chiku aliangalia mbele yake akamuona mama yake na mwalimu Doka wameketi, moja kwa moja alienda kwa mama yake akamuuliza, kwa nini tupo hapa? Tina alimwambia Chiku amsalimie kwanza mwalimu wake akamsalimia kisha akaendelea kumuuliza mama yake, mama! tumekuja kufanya nini hapa? mwalimu Doka alimuita, Chiku akamwambia subiri ule chakula alafu mama atakujibu maswali yako, Chiku alimsikiliza mwalimu wake akaketi kwenye kochi na chakula nacho kilikwishakuwa tayali, wakala kwa pamoja walipomaliza, Bite alimchukua Chiku akamuogesha, alipomaliza tu Chiku alipitiwa na usingizi mzito na mwalimu Doka nae akapata nafasi ya kumuuliza Tina ni kipi kimemsibu, Tina alieleza yote yaliyompata na yale yote ambayo shemeji zake walivyomfanyia, mwalimu Doka alihuzunika sana na alimuahidi Tina kuwa atakuwa nae bega kwa bega katika kuhakikisha kuwa nyumba anaipata.


SEHEMU YA TATU
          Mwalimu Doka alipeleka taarifa kwa mwalimu mkuu juu ya matatizo aliyoyapata Tina rambirambi zilichangishwa kwa waalimu pamoja na wanafunzi, wakapata jumla ya shiringi laki moja na nusu moja kwa moja mwalimu doka alimsaidia Tina kutafuta nyumba ya kupangia akafanikiwa kupata nyumba  iliyokuwa pembezoni mwa shule, vilevile alimuomba mkewe amsaidie Tina vyombo  viwili vitatu ambavyo vitaweza  kumsaidia na kuna baadhi ya waalimu wengine walimpatia Tina  vitu mbalimbali wengine walimpa vyombo, wengine walimpa nguo na mwalimu mkuu alimpa kitanda na godoro, lakini yote haya yalikuwa ni matunda ya mume wake ambae alikuwa na ushirikiano na wenzie, Tina alimshukuu sana mwalimu Doka na mkewe pamoja na wale wote ambao wamemsaidia kwa namna moja ama nyingine, Tina alienda kuyaanza maisha mapya, mwalimu Doka alienda  kituo cha polisi kueleza jambo ambalo tina limempata na uchunguzi ulianza mara moja !,Tina nae hakuwa nyuma nyuma, alianzisha biashara ya mkaa ambayo ilimpatia fedha za kukidhi mahitaji yake madogo madogo, watu wote mtaani walimtambua, kutokana na maneno yake mazuri kwa wateja wake, watu kutoka mitaa mbalimbali walimiminika kwa mama Chiku kuhitaji mkaa, Tina alifuahi sana na maisha yake yalipiga hatua siku hadi siku, alimjali sana mtoto wake, alimwamsha mapema kwa ajili ya kuwahi shule, alimpenda sana mtoto wake kwani yeye alikuwa ndilo tegemeo lake la mwisho na ndugu yake wa pekee, Chiku nae alikuwa ni mtoto mwenye adabu, heshima na niddamu ya hali ya juu kwa waalimu wake na mama yake pamoja na watu wote waliomzunguka, waalimu walimpenda sana Chiku alifanya vizui katika masomo yakeke, kitu ambacho kilimfanya mama yake awe na furaha muda wote na aone kuwa bado mume wake yu pamoja na yeye katika kumpa malezi bora mtoto wao  wa pekee. Tina hakuishiwana hamu ya kumpa mwanawe maneno ya kumpa faraja, ambayo yatamsahauisha upweke alioachiwa na baba yake pamoja na ule ubaya aliofanyiwa na baba zake wadogo.
        Ilikuwa ni siku ya kufunga shule, siku ambayo Chiku alipewa Zawadi kwa kushika nafasi ya kwanza katika Darasa lao, lakini hakuzifurahia Zawadi zile kwasababu alimkumbuka sana baba yake pale ambapo alifanya vizuri katika masomo yake alimpeleka sehemu yenye miti mizuri yenye vivuli vya kuvutia na kuanza kumsimulia hadithi nzuri zenye kuvutia lakini leo hii alijiuliza ni nani ambae atamfanyia yote yale ambayo  baba yake alikuwa akimfanyia aliishia kububujikwa na machozi alirudi nyumbani hali ya kuwa hana  furaha, mama yake alimuuliza ni kitu gani kinamkosesha furaha, Chiku alianza kulia huku akimpa mama yake ripoti ya matokeo pamoja na Zawadi alizopewa Tina aligundua kitu, haraka akaingiza ndani makopo ya mkaa akamchukua chiku wakaelekea sehemu ambayo baba yake alikuwa anampeleka walipofika Chiku alisahau yote alifurahi sana na kujihisi yupo na baba yake kipenzi, akamuahidi mama yake kuwa atampenda na atamtunza kadri ya uwezo wake, jua lilipoanza kuzama   Tina na mwamawe wakaondoka, walipofika nyumbani, Tina aliandaa chakula kizuri kwa ajili ya mwanawe, na Chiku nae alikifurahia chakula basi furaha ilitanda ndani ya nyumba ile


SEHEMU YA NNE

Chiku alipokuwa likizo alimsaidia mama yake kazi ndogondogo, katika muda ule wa likizo Tina alianzisha mradi wa matunda, Chiku alikuwa anazunguka mitaani kuuza matunda na mama yake alikuwa anabakia nyumbani anauza mkaa, Chiku alishazoea maisha ya kuzunguka mtaani ingawa kuna baadhi ya wanafunzi wenzake ambao walikuwa wanamcheka na kumpa jina la “MTOTO WA MTAANI’’   lakini yeye hakujali  kwa sababu alikuwa ana nia ya kumsaidia mama yake jua, mvua vyote viliishia mwilini mwake, lakini hakuchoka hata siku moja kila alipoamka asubuhi alichukua beseni lake la matunda na kujichanganya mtaani , Chiku alikuwa ni mtotpo mdogo wa Darasa la tatu lakini alifanya kazi ambazo zilikuwa si za kuzifanya yeye ila tu ilimbidi afanye hivyo hivyo, hata Tina nae hakupenda mtoto wake aishi katika mazingira yale lakini atafanyaje hali ya kuwa hana uwezo wa kumpa starehe ambazo watoto wengine wanapewa na wazazi wao .
         Siku moja Tina na mwanawe Chiku walikuwa wanakwenda sokoni Kufuata matunda ya biashara, ghafla Tina alimuona shemeji yake Kangomba, Tina alishtuka akajitahidi kumzuia mtoto wake ili asimuone baba yake mdogo kwani akimuona atakumbuka machungu ambayo yameshapita, Kangomba alimwona Tina na mwananawe, akasema, Mmh! Huyu kahaba bado yupo? Inabidi nimpe taarifa bwana mkubwa ili tumshughulikie aondoke. Tina na Chiku walinunua matunda wakaondoka.  Kangomba aliwafuatilia nyuma bila ya wao wenyewe kujua akapafahamu wanapoishi, bila kuchelewa Kangomba alienda kwa kaka yake akamueleza kile alichokiona na akamuambia kuwa kama wakimuacha Tina aendelee kuishi katika maeneo yale atawasababishia matatizo, walikubaliana waende kwa Tina wakamfanyie kitu ambacho hatokuja asahau katika maisha yake, ghafla mlango uligogwa ngo! ngo! ngo! Sunga alinyanyuka akaenda kufungua mlango, alipofungua akaona watu wanne wamesimama mlangoni, Sunga aliwauliza niwasaidie nini? Mmoja kati yao akaonesha kitambulisho kisha akasema, mimi ni askari, unahitajika kituo cha polisi mara moja, huku ndani Kangomba aliposikia mambo ya askari, akaogopa sana kisha akachungulia dirishani akawaona watu wanne lakini kati yao alimfahamu mmoja ambae ni mwalimu Doka kwa sababu alikuwa akimuona kwa kaka yake Alfani wakati wa uhai wake, akaona imesha kuwa balaa akafungua mlango wa nyuma akakimbia, bwana Sunga alijaribu kuuliza nini kimetokea lakini aliambiwa ataenda kujua huko huko, askali wawili wakaingia ndani wakaangaliaangalia hawakufanikiwa kukuta mtu, wakatoka nje wakamchukua bwana Sunga wakampeleka kituoni,  Kangomba alipofika nyumbani kwake alijiuliza ni kwa nini mwalimu Doka ameamua kumsaidia Tina lakini akasema ndani ya usiku wa leo lazuma nipoteze ushahidi wote, akaandaa kikosi cha watu kumi wenye nguvu akawapa fedha na akawaambia wakamsambaratishe mwalimu Doka wakimaliza wakafanye fujo kwa Tina na wakiweza wamuue yeye pamoja na mtoto wake, majira ya saa saba usiku walienda moja kwa moja kwa mwalimu Doka wakaeeneza petroli katika kila pembe ya nyumba ille wakawasha moto maskini mwalimu Doka na mke wake walijaribu kuokoa maisha yao lakini walishindwa, moto ulienea nyumba nzima na nyaya za umeme zikadaka moto na kusababisha shoti ambayo iliwamaliza moja kwa moja, majirani walifanya jitihada  za kuokoa maisha yao lakini walishindwa, lile kundi la vijana kumi wakiongozwa na Kangomba wakaenda moja kwa moja hadi kwa Tina mmoja wao akagonga mlango, ngo! ngo! Tima alijikurupua kitandani, mlango ukagogwa tena, ngo!ngo!ngo! Tina aliuliza kwa uoga ni na………na…..ni wewe? Yule kijana akajibu ni mimi apa nahitaji mkaa ! mkaa usiku kama huu? Tina aliuliza tena, ndio dada yangu nina mgojwa anahitaji kula sasa tumeishiwa na mkaa, Tina aliogopa lakini kutokana na moyo wa huruma aliokuwa nao  akafungua mlango, alipofungua mlango alishangaa  kuona kipande cha mtu kimesimama mbele yake punde si punde kundi la watu ambao walivalia mavazi meusi likamvamia wakamfunga kitambaausoni, wakamlaza chini wakamvua nguo wakamuacha kama alivyozaliwa wakaanza KUMUASI, mmoja baada ya mwingine, Tina alijaribu kupiga yowe lakini sauti haikutoka kwa sababu walikwisha mfunga kitambaa usoni, walimfanyia tendo la kinyama kila mmoja alimuingilia anavyotaka, kisha wakaondoka. Tina alilia sana, akajuta ni kwa nini alizaliwa katika dunia hii, akaona ameshapoteza thamani katika maisha yake ,akahisi amepoteza heshima yake yote alitamani afe kuliko kuishi akajalibu kujiinua pale alipolala lakini alishindwa alihisi maumivu makali katikati ya mapaja yake, damu zilimtoka hadi akaishiwa na nguvu akapoteza fahamu, kulipopambazuka,  Chiku aliamka akashangaa kuona yupo peke yake kitandani, alidhani kuwa mama yake yupo nje anaendelea na biashara yake ya mkaa, lakini aliyaona makopo ambayo mama yake anatumia kupimia mkaa, akadhani kuwa labda atakuwa amefuata matunda sokoni, alipotoka nje alimuona mama yake yupo uchi na,mwili mzima zimemjaa damu, aliogopa sana akawahi ndani kuchukia nguo na kwenda kumsitili mama yake alijalibu kumuamsha mama yake lakini hakuamka. Chiku alilia saana majirani walikimbilia kule alipo Chiku walipofika wakashangazwa na kile walichokiona  bila kuchelewa wakamuwahisha hospitalini, Chiku alibaki nyumbani wakati hana amani, alilia sana mpaka sauti ikamuishia, ghafra  mlango uligogwa, ngo !ngo! ngo! Alipotoka nje alimkuta rafiki yake anaeitwa Emma analia akamuuliza kwa nini unalia? Akamuambia kuna taarifa mbaya mwalimu Doka na mke wake wamefariki,  wamefariki? Chiku aliuliza kwa mshangao, akadondoka chini akapoteza  fahamu, Emma alipiga kelele kwa ajili ya kutaka msaada, muda uleule kuna mama mmoja alikuwa amekuja kwa mama Chiku kuhitaji mkaa lakini alimkuta Chiku yupo katika hali mbaya akamuwahisha hospitalini alipofika alishangaa kuona na Tina nae yupo hospitali , 
      Masaa matatu yalipita Tina na mwanawe walikuwa hawajapata fahamu, majrani walihuzunika sana  kwa kitendo alichofanyiwa Tina  lakini watu walijua moja kwa moja kuwa Kangomba ndie aliyefanya yote na kuna mmoja wao akasema kuwa ameokota pochi ndani yake kuna vitambulisho vya Kangomba, taarifa zilifikishwa kituo cha polisi na harakati za kumtafuta zikaanza,Tina na mwanawe walipata fahamu madaktari wakajitahidi kutoa matibabu kwa wawili wale hadi wakapona, lakini Tina hakuona tena thamani ya yeye kuendelea kuwa hai  pale tu aliposikia kuwa mtu ambae alikuwa ni msaada mkubwa kwake, aliyemsaidia kupigania haki yake amepoteza maisha, akikumbuka na ule unyama aliofanyiwa akuona haja ya yeye kuendelea kuishi katika dunia iliyojaa uozo na uchafu wa kila aina, lakinipia alipata hamu ya kuishi pale alipomuona Chiku, marafiki zake walijitahidi kuwa karibu nae na kumpa moyo lakini alihisi bado anadharaulika kwa kile alichofanyiwa, baada ya siku kadhaa Kangomba alikamatwa akapelekwa kituo cha polisi, Tina nae aliitwa kituoni kwa ajili ya kuhojiwa, alipofika alishangaa kuwakuta shemeji zake kituoni walipo muona tina walijaribu kuficha sura zao lakini hawakuweza,Tina alihuzunika sana, pale tu alipoambiwa shemeji yake ndie amemfanyia unyama wote ule. Tina aliogopa sana akaangua kilio huku anasema, ni wewe kweli ? kwa nini laki umeamua kunifanyia jambo baya Kiasi kile? Nimekukosea nini mimi? au nilifanya makosa kuolewa na Ndugu yenu? kwani lakini mmekuwa wabaya kwangu? Mmenidhulumu mali za mume wangu na mimi pia mnataka muniuwe? Kangomba alishikwa na aibu, alijikaza lakini alishindwa akadondoka chini pu! Sunga nae alipata mshtuko kwa kuona mdogo wake amedondoka, palepale na yeye alidondoka chini pu! Tina alishangaa akapatwa na woga na huruma ulimjaa akasema, nimewasamehe  jamani sitaki mufe kwa ajili yangu, lakni wapi! Wote walipoteza maisha palepale,Tina alilia sana akapoteza muelekeo, mahakama ilijaribu kumsaidia Tina kupata  mali zake lakini kumbe vilishauzwa na shemeji zake, Tina alilia sana mwisho akaona amshukuru Mungu kwa yote yaliyotokea.


SEHEMU YA TANO
Chiku sasa amekua msichana mkubwa amemaliza elimu yake ya Msingi anasubiria majibu ili aweza kujiunga na elimu ya sekondari. Kwa upande wake maisha yalikua magumu kila kunapokucha, mama yake sasa ameacha kufanya biashara ya mkaa kwa sababu imemuathiri kiafya imemsababishia ugonjwa wa kifua, hivyo hawezi tena kufanya biashara hiyo. Vilevile hata kutembea kwa umbali mrefu hawezi tena, kifua kikianza kumbana anakohoa hadi damu zinamtoka mdomoni. Chiku aliendeleza biashara ya matunda na mbogamboga ambayo ingeweza kumsaidia katika matumizi madogo madogo lakini haikumsaidia kwa kua pesa zote alizozipata ziliishia kulipa kodi ya nyumba ambayo wanaishi.
            Siku moja Tina alienda kwenye mizunguko yake kama ilivyo ada yake kuuza matunda na mboga mboga wakati yupo njiani alikutana na mvulana ambaye alisoma nae yule mvulana aliita Chikuuu! Chiku akageuka kisha akasema waaooo! Hee! Umemaliza shule ndo umenenepa kiasi hiki? Yule kijana aliyejulikana kwa jina la Jelia alimkejeli kwa kumwambia naona wewe ndo umekua mrembo kama angle. Mmhh!! Ebu acha kunikejeli wewe, Chiku alimjibu kwa sauti iliyojaa aibu. Chiku alisogea kwenye kivuli cha mti pembezoni kidogo na barabara, na Jelia alisogea karibu ya Chiku kisha akamwambia majibu ya mtihani yemetoka, katika Darasa letu tumefaulu watu watano tu! Chiku aliuliza kwa shauku na mimi nimefaulu? Jelia alimjibu ndio umefaulu unatakiwa kuripoti shule hivi karibuni, vipi na rafiki yangu Emma? Yeye hajafaulu Jelia alimjibu, katika hao msichana ni peke yako. Chiku alifurahi sana ila alijua hatoweza kwenda shule maana mama yake hakua na pesa za kumpeleka shule, Chiku alimwambia jelia basi acha mimi nirudi nyumbani nikampe mama taarifa, wakaagana kwa furaha isiyo na kifani. Chiku aligeuza na kupelekea nyumbani kwao, alipofika nyumbani alimkuta mama yake imemuanza homa yake ya kifua, anakohoa kikohozi cha damu, ameishiwa nguvu na anatapatapa mithili ya kuku anayetaka kutaga, mama!! Chiku aliita kwa mshangao, akaangalia mkono wake akaona ana Shilingi elfu tatu tu za kitanzania na ndani alikua na akiba ya Shilingi elfu kumi na tano ambayo ndio pesa ya kulipa kodi ya nyumba, akawaza kisha akaona ni bora amuwaishe mama yake hospitali, haraka akaita bajaji, tayari kwa kumpeleka mama yake hospitali, punde si punde waliwasili hospitali haraka Tina alipelekwa katika chumba maalumu na kuanza kupatiwa matibabu, ila kifua kilikua kimembana sana mpaka akashindwa kupumua vizuri, Tina alimuomba Chiku aongee nae maneno mawili matatu, Chiku aliwahi ndani akamkuta mama yake anapumua kwa shida sana, Chiku alimwuliza mama yake, vipi hali yako? Tina alimjibu mwanae, mwanamgu nimekata tama ya kuishi naona muda unasogea na hali inakua tete, siwezi kupona tena, ila nakuomba uwe mwanamke jasiri, mtulivu, msikivu, mnyenyekevu na mwenye huruma kwa kila mtu unayemjua na usiyemjua, mkubwa na mdogo, Chiku alilia sana huku anamwambia mama yake, mama nimefaulu mwanao! Nahitajika kuripoti shuleni hivi karibuni, Tina alizidi kupumua kwa shida sana kisha akamshika mwamawe mkono palepale akapoteza maisha, Chiku alilia kwa uchungu wa hali ya juu, aliumia sana, aliwaza ni nani ambae atamsaidia, nani ambae atamhurumia na ni nani ambae atamshauri pale atakapopatwa na matatizo. Basi harakati za mazishi zikafanyika, kutokana na ukarimu aliokua nao Tina katika uhai wake alizikwa na wanakijiji, ilihali hakuwa na Ndugu hata mmoja katika kijiji kile ispokua mtoto wake tu! Chiku alihuzunika alikosa amani katika maisha yake kila alipomkumbuka mama yake alikosa furaha na pale aliporudisha mawazo yake nyuma alimkumbuka baba yake kipenzi bwana Alfni, alikosa furaha japo kua majirani walijitahidi kumfariji ili aweze kusahau yale yaliyotokea lakini chiku katu hakuweza kurudisha furaha yake ya asili. Walimu wa shule ya msindi aliyosoma walimpa moyo pia wanafunzi ambao alihitimu nao Darasa la saba walimpa moyo, ila Chiku hakurudi katika hali yake ambayo watu walizoea kumuona.


SEHEMU YA SITA
            Mwezi mmoja sasa tangu Tina ameaga dunia, maisha ya chiku yalienda ndivyosivyo kila jua linapochomoza aliona bora ya jana kuliko leo, alipewa taarifa kua amechaguliwa kujiunga na shule ya sekondari Kazimoto iliyopo wilayani Masasi lakini hakua na pesa zitakazomwezesha kuendelea na masomo hayo, alijaribu kuomba msaada katika sehemu tofauti, waalimu nao walijitahidi kutafuta wafadhili ambao wangeweza kumsomesha yatima huyu lakini jitihada zote ziligonga mwamba, mpaka wanafunzi wote wakapelekwa mashuleni na wazazi wao, muda wa wanafunzi kuripot shule ukaisha na habari ya Chiku kusoma zikaishia hapo.
            Chiku aliendeleza biashara yake ya mbogamboga na matunda kijiji kizima alijulikana kwa ujasiri na ukarimu wake watu walimpenda sana, alikua na kauli nzuri kwa wateja wake vilevile alimheshimu kila mmoja mwenyeji na mgeni wakubwa kwa wadogo wanawake kwa wanaume, maisha yaliendelea hivyo hivyo akipata anakula akikosa analala.
            Siku moja Chiku hakwenda kwenye biashara zake alipumzika nyumbani, akafanya usafi wa chumba chake pamoja na Mazingira yaliyozunguka nyumba ile, alipomaliza akaandaa chakula akala, wakati anakula alikumbuka malezi ambayo marehemu mama yake alimpa alijikuta anatokwa na mchozi, ghafla mlango uligongwa, aliogopa kisha akakumbuka kilichomkuta mama yake, lakini alijipa moyo kwa kua ilikua mchana kweupe. Akafungua mlango, akashangaa kuona vijana wawili wameingia ndani na yeye akasukumizwa ndani kisha vijana wale wakafunga mlango. Walimvamia na kumfunga kitambaa cheusi usoni kijana mmoja alimziba mdomo Chiku mwengine akaanza kumvua nguo, chiku alijaribu kujitoa mikononi mwa wawili wale lakini hakuweza, kijana mmoja akamwambia mwenzie anza alafu mimi nitafuatia, akafungua zipu ya suruali yake, yele aliyemziba mdomo Chiku akaona mwenzie anachelewa akamwachia, ili aanze yeye, palepale Chiku akapata mwanya, haraka akotoa kitambaa usoni, karibu yake kulikua na chupa ya soda akaishika kwa nguvu akamrushia mmoja wao ikampiga kichwani, kijana aliyebakia alisahau yaliyomleta pale akaanza kushughulika na mwenzie aliyezimia kwa kipigo alichopokea kutoka kwa Chiku. Chiku alichukua kipande cha chupa ile iliyovunjika akamchoma nayo kijana Yule katika jicho lake, alipiga makelele kama paka aliyepigwa kwa kosa la kuiba kitoweo, Chiku aliogopa akachanganyikiwa na hakuamini kama mikono yake ndio imefanya tukio lile. Haraka alivaa nguo akachukua begi lake la nguo na kipochi chake chenye fedha akaangalia nje akagundua hakuna mtu akatimua mbio mpaka stendi ya mabasi alipofika hakuchelewa aliingia ndani ya gari na gari ilikua tayari imeshapakia abiria ikachapa mwendo, yumo ndani ya gari machozi yalimbubujika, abiria wote waliokua ndani ya gari lile walimkodolea macho lakini yeye hakujali.  Lakini aliwaza wapi atakwenda kufikia, ili hali yeye hajawahi kwenda mjini hata siku moja na hana anayemfamu hana Ndugu wala rafiki, lakini alijiamini na akakumbuka wosia aliopewa na marehemu mama yake kua siku zote awe jasiri na mwenye kujiamini.
            Ilipofika saa moja na nusu usiku gari liliwasili jijini Dar es salaamu abiria walishuka Chiku naye akashuka kila mtu aliingilia upande wake wapo waliokodisha taksi wengine bajaji na wengine bodaboda wawafikishe majumbani mwao. Chiku hakuelewa aingilie wapi, alishangaa shangaa tu mara aangalie huku mara kule akakiona kinjia kidogo akasema subiri nifate njia hii, wakati anafuata njia ile kuna vibaka wawili wakawa wanamfuata kwa nyuma, Chiku alihisi kuna watu wanamfuata aliongeza mwendo akagundua kua na wao wanaongeza mwendo, Chiku alitimua mbio kule anakoelekea kulikua na barabara kubwa ya magari, ile anataka kuvuka barabara kuna gari lilikua linatembea kwa kasi likamzoa yeye na begi lake begi lake la ngua likarukia mtaroni dereva wa gari alifunga breki ghafla wakashuka mwanamke na mwanaume, wakamnyanyua wakamuweka ndani ya gari wakamuwahisha hospitalini. Chiku alipatiwa matibabu mpaka akapona, akawa katika hali nzuri, huku kijijini taarifa za kutoroka Chiku zilisambaa na wale vijana wawili waliotaka kumnajisi Chiku walipoteza maisha na hakuna aliyehangaika kuhoji juu ya vifo vyao kwa sababu walijulikana kwa tabia chafu.


SEHEMU YA SABA
            Baada ya chiku kupona alichukuliwa na wawili wale moja kwa moja mpaka nyumbani kwao, walipofika wakamkaribisha vizuri, akapewa chakula, alipomaliza aliwashukuru kwa yale yote waliyomsaidia, baadae utambulisho ulianza, mimi nimaitwa Toni na huyu ni mke wangu anaitwa Janeth sijui wewe unaitwa nani? Naitwa Chiku, unaishi wapi? Toni aliuliza Chiku alijibu kwa unyonge naishi…………. Akasita kidogo kisha akaanza kutokwa na machozi huku anasema ni historia ndefu sana, aliwasimulia yote yaliyomkuta hadi kufikia hatua ya yeye kukimbilia mjini. Toni na Janeth walimhurumia sana kwa yale ambayo yamemkuta hali ya kua bado ni mtoto mdogo. Wakamuahidi kumsaidia kwa yale ambayo yako ndani ya uwezo wao, walimnunulia nguo nzuri na viatu vizuri na wakamtafutia shule akajiunga kidata cha kwanza.
            Chiku ni mtoto ambae alikua na nidhamu kwa walezi wake pamoja na waalimu wake, furaha ilirejea taratibu, Toni na Janeth walijitahidi kumpa Chiku mahitaji yote ambayo yanahitajika kwa mtoto, Chiku nae alijitahidi kuwa mtiifu kwa walezi wake wapya.
            Kutokana na maisha mazuri aliyoishi Chiku kwa muda ule, urembo wake ulijidhihirisha alikua ni mrefu wa wastani mwenye umbo namba nane, pua yake ndefu kidogo na macho yake yalikua ni makubwa kidogo ya uduara yalimvutia kila aliyemuangalia nguo za shule zilimkaa vizuri hadi wasichana wenzie wakamuonea wivu, wavulana wengi walijipitisha karibu ya Chiku lakini Chiku alikua kafundwa akafundika hakuwa na tabia chafu ambazo wasichana wengine walikua nazo. Alijituma kadiri awezavyo katika masomo yake waalimu walimpenda sana Chiku.
            Siku moja wakiwa darasani, mwalimu alikua anafuindisha somo la hisabati, Chiku alikua makini sana kumsikiliza mwalimu, kuna mvulana mmoja aliyeketi karibu na Chiku alionekana kumuangalia sana binti yule kwa jicho la wizi, mwalimu akagundua akaita wewe kijana njoo utufanyie swali moja hapa ubaoni, kijana alishtuka ila alijikaza akanyanyuka na kwenda ubaoni kujaribu kufanya swali aliloambiwa alifanye. Kwa sababu ya kutokua makini kusikiliza alishindwa kufanya swali, Chiku alonyoosha mkono ishara ya kutaka kwenda kumsaidia yule kijana, mwalimu alimpa nafasi Chiku, Chiku alinyanyuka na kuelekea ubaoni akalifanya swali vizuri na kwa usahihi wake, very good mwalimu alimpongeza Chiku na akawashauri wanafunzi wengine waige tabia na mienendo ya Chiku.  Wakati chiku anaelekea kwenye kiti chake mwalimu alijikuta anamuangalia Chiku kwa umbo lake zuri ambalo amejaaliwa na mungu mwisho akasema someni….. someni…. Someni saana wanafunzi kisha akaondoka
            Kengele ya kurudi nymbani iligongwa, kama kawaida ya Chiku kengele ikisikika tu huwa hana mambo mengi anayoyafanya zaidi ya kuchukua begi lake la madaftari na kwenda kumsubiria Toni amfuate ili amrudishe nyumbani, wakati anamsubiria Toni aje na usafiri kuna kijana mrefu ambae alikua kidato cha tatu alimsogelea Chiku kisha akamsalimia, Afternoon miss, Chiku alimjibu Afternoon how are you? Yule kijana alianza kuropoka kwa majina ninaitwa Kilian John Mgalula ni kaka mkuu katika shule hii ya St. Joseph, chiku alimjibu Oooh! Nimefurahi kukufahamu, punde si punde Toni alifika na gari yake Chiku akaingia ndani ya gari na kumuacha Yule kijana mdomo wazi, Toni aliwasha gari hao wakaondoka. Kijana alijihisi amedharauliwa ile anageuza shingo yake tu macho kwa macho akakutana na msichana anayeitwa Anna alikua amekasirika kisha akasema Kilian umekosa nini wewe mwanaume mpaka umfate bint mdogo wa kidato cha kwanza, mwangalie mvulana umekosa haya wewe!! Au kwa kua mimi baba yangu hana gari, ujue Kilian unauumiza moyo wangu. Kwa dharau kilian alimjibu Anna kuanzia leo usinijue, mwanamke gani wewe mfupi kama kipande cha sabuni, mwanamke mshamba mshamba kaa mbali na mimi, kisha huyo akaondoka. Anna alikaa chini taratibu akalia kwa uchungu baadae alinyanyuka akaondoka.


  SEHEMU YA NANE
Chiku alionekana kua ni mtoto bora, mtiifu, Mwaminifu na mkarimu kila kunapokucha, waalimu walizidi kuvutiwa na tabia za Chiku, walezi wake pia walimwamini na wakamwona kama mtoto wao wa kumzaa. Chiku ni msichana ambaye anajituma kila anapoamka asubuhi anasafisha chumba chake, anaosha vyombo na kudeki nyumba nzima, akimaliza anajiandaa kwa ajili ya kuwahi shule. Anapokua shule hapendi kujichanganya na makundi mabaya ambayo yatamharibia maisha. Siku moja Chiku alikua ameketi chini ya mti wenye kivuli kizuri uliopo katika Mazingira ya shule akiwa amefunua kitabu chake cha tamthilia anasoma, ghafla aliona kundi la wasichana wapatao saba wa kidato cha tatu wanakuja pale alipo, walipofika tu bila ya salaam wakaanza kumshambulia kwa maneno machafu na matusi, mmoja wao aliyejulikana kwa jina la Anna alimwambia Chiku, wewe mtoto kaa mbali na Kilian, usipofanya hivyo utanijua mimi ni nani? Akampokonya kitabu akakichana chana akamrushia usoni, Chiku hakusema chochote alikaa kimya, mmoja wao akasema yaani huyu mtoto anaonekana ni kiburi sana mwangalie kwanza macho yake yalivyo. Wasichana wale waliondoka, Chiku alilia kwa hasira lakini hakupenda ugomvi, sio kama alishindwa kuwatemea maneno machafu, lakini kutokana na nidhamu aliyonayo alitulia kimya, wakati tukio lile likiendelea Kilian alikua anashuhudia kile kilichotokeo alijibanza kwenye ukuta wa Darasa na akashuhudia yote. Kilian alimuhurumia sana Chiku, akaona aende moja kwa moja hadi kwenye ofisi ya nidhamu akatoe taarifa, alipofika alimkuta mwalimu ameketi kisha akamueleza yote, mwalimu alisema nyie ndio viongozi ambao tunawahitaji katika shule yetu. Punde si punde kengele ya dharula ikagongwa wanafunzi wote wakakusanyika paredi, kaka mkuu ambaye ni Kilian aliwaamuru wanafunzi wanyamaze kwan kuna tangazo kutoka kwa mwalimu wa nidhamu. Mwalimu wa nidhamu alianza kwa kuwasalimia wanafunzi kisha akasema wafuatao wapite mbele! Akaita majina ya wasichana saba kisha akawaambia wapige magoti mbele ya wanafunzi wenzao, kisha akamuomba Chiku nae aje mbele, Chiku aliogopa akaanza kububujikwa na machozi, wakati anaenda mbele wanafunzi wote walimkodolea macho, waalimu nao hawakuweza kuyazuia macho yao yasimtazame Chiku, walimuangalia mtoto jinsi anavyotembea , na umbo lake jinsi lilivyokua la kipekee na sura yake ilimvutia kila aliyemwangalia, alipofika mbele, mwalimu wa nidhamu alisema hawa asichana saba wamemshambulia kwa matusi binti huyu ambaye hana hatia, wanafunzi wote walishangaa, Chiku nae alishangaa taarifa zimefikaje kwa mwalimu? Hivyo basi tutawatandika fimbo tatu tatu kila mmoja ili iwe funzo kwa wengine na mwisho tutaweapa barua waendenazo kwa wazazi wao. Mwalimu Yule alichukua fimbo akawatandika kama alivyosema na kisha akawapa barua, hao wakaondoka. Kuanzia siku hiyo wanafunzi walimuheshimu Chiku hakuna ambaye alitaka kumuonea, kwa upande wake Chiku siku hiyo hakua na amani hata kidogo, hata pale Toni alipomfuata aligundua kuwa Chiku hakuwa na furaha. Walipofika nyumbani, Toni na Janeth walijaribu kumuuliza Chiku kwa nini hana furaha? Akawarleza yale yote yaliyotokea. Toni na Janeth walijaribu kumfariji Chiku, na hakuchukua muda akarudi katika hali yake ya kawaida.


SEHEMU YA TISA
            Katika maisha ya shule Chiku alikumbana na changamoto nyingi sana lakini alijitahidi kupambana nazo, baadhi ya waalimu wenye tabia chafu walijaribu kumrubuni Chiku, lakini Chiku alikua na malengo yake. Alipokua kidato cha pili alishika nafasi ya kwanza ya kwanza katika mkoa wa Dar-es-Salaam, shule ilimzawadia kwa kuipa shule hiyo sifa nzuri, lakini pia alipata Zawadi nyingi kutoka mkoani, walezi wake pia walipewa Zawadi kwa matunzo mazuri ya mtoto wao, aliingia kidato cha tatu akiwa na furaha tele moyoni. Mara kwa mara waalimu walimuomba Chiku awashauri wanafunzi wenzake katika masomo, Chiku alijaribu kupanga ratiba yake vizuri ili aweze kuwasaidia wenzie, lakini alihitaji kupata muda wa ziada ambao angeutumia kujisomea mwenyewe maana muda mwingi aliutumia kuwasaidia wenzie. Chiku aliwaomba walezi wake abakie shule kwa muda wa masaa mawili pale ambapo wenzie wanarudi nyumbani ili aweze kujisomea, kwa kua walezi wake hawakua na shaka nae aliruhusiwa lakini walimshauri awe makini. Chiku alifurahi kuona walezi wake wanamuamini na kujali anachokihitajia, siku moja Chiku alikua amebakia darasani peke yake wakati wanafunzi wote wamekwishaondoka, akajikuta amemkumbuka marehemu mama yake, taabu na shida zote alizopitia wakati yu mdogo akajikuta atabubujikwa na machozi, wakati Chiku analia kuna mwalimu alikua anapita nje akahisi kuma kuna sauti inatoka ndani ya Darasa, ikibidi aangalie ni nani ambaye yumo ndani, alipofika alishangaa kumuona Chiku ambaye alikua anamtafuta na kumsaka kwa muda mrefu, taratiibu akaingia kisha akamziba macho, Chiku aliogopa sana, Yule mwalimu akasema usiogope ni mimi, Chiku alipogeuka alikutana macho kwa macho na Yule mwalimu, Chiku alichukia akasema, mwalimu kwa nini lakini haujiheshimu, Yule mwalimu alimjibu hivi  mpaka leo unaniita mwalimu, niite jina langu bwana, mimi ninaitwa Sheby. Mmh !! Chiku aliguna kisha akakusanya madaftari yake na kuyaweka ndani ya begi akanyanyuka na kuanza kuondoka, mwalimu Shebi alimshika mkono Chiku kisha akachomoa kitita cha fedha mfukoni akampa kisha akamwambia nifikirie. Chiku alizipokea zile fedha kisha akamrushia usoni, akamwambia thamani ya utu wangu hailingani na hivyo vijisenti vyako kisha huyo akaondoka.
            Mwalimu alihisi amedharaulika kisha akajilaumu ni kwa nini alimfuata binti Yule, lakini alijisemea kimoyomoyo nitampata tu! Nitafanya kila mbinu hadi nipate ninachokitaka, walikuapo wengi wanaofanana na yeye lakini leo wako wapi mbona nilishawapata? Nitampata tu hata kama isiwe mwaka huu. Chiku alielekea barabarani dakika chache tu na Toni nae alimfuata, kisha aliingia kwenye gari hao wakaondoka, Sheby nae hakuchelewa akaondoka.


SEHEMU YA KUMI
            Mwalimu Sheby hakuchoka kumfuatilia Chiku, alijitahidi kumpa maneno ya kila aina lakini Chiku alikua mgumu kama kisiki cha mpingo, aliyasikiliza maneno yake lakini hakuyazingatia hata kwa udogo wa mdudu Chungu. Lakini mwalimu sheby hakukoma, Siku moja kulikua na kikao baina ya waalimu na wanafunzi wote wa St. Joseph. Cha kushangaza waalimu wote waliende kwenye kikao na wanafunzi wote walikua kwenye kikao ila mwalimu Sheby tu alibakia ofisini. Kwa mbali alimwona mwanafunzi akielekea waliko wenzake, akamwita kisha akamwambia naomba ukaniitie Chiku mwambie anaitwa katika ofisi ya taaluma, yule mwanafunzi alifikisha taarifa kama alivyoagizwa. Chiku alifikiri kwa muda kidogo ni kipi aliitiwa katika ofisi ya taaluma, alikua na wasiwasi wa hali ya juu kisha akanyanyuka na kuelekea kule alipoitwa, alipofika aligonga mlango, mlango ulifunguliwa akaingia ndani, alipoingia tu mwalimu Shebi alifunga mlango na funguo akaweka mfukoni, Chiku akashangaa kisha akauliza mwalimu mbona unafunga mlango? Mwalimu Shebi alitabasamu kisha akasema ina maana wewe hujui, bila kuchelewa mwalimu Yule alimshika Chiku mabega akamgandamiza ukutani kisha akamwambia kwa muda mrefu nilikua nakutafuta! Nafasi hii siamini kama leo nimeipata, Chiku alitetemeka kama amepigwa shoti ya umeme, akaseme mwalimu mimi sihitaji unachohitaji wewe naomba uniache niondoke, mwalimu shebi alitabasamu huku anaupapasapapasa mgongo wa Chiku, Chiku alihamaki akapiga kelele lakini wapi kelele zake ziliishia ndani ya ofisi ile tu na nje haikutoka hata herufi ya sauti kwa kua ofisi ile ilikua na madirisha ya vioo. Mwalimu Shebi alijaribu kutaka kumnajisi mwanafunzi wake lakini mwanafunzi pia hakua nyuma Kutumia ujasiri alonao kujinasua katika mtego ule. Ama kweli mapenzi ni upofu, ububu na upofu, mwalimu hakuona kua yupo ndani ya ofisi hakusema neno lolote na wala hakusikia kilio na kelele za Chiku alichanganyikiwa akanza kumvua Chiku nguo kwa nguvu lakini Chiku alijitahidi kumzuia, mwalimu Shebi alivuta shati la Chiku kwa nguvu hadi akalichana akabakiwa na kitopu ambacho kimemsitiri kifua chake, looh! Mwalimu alizidi kuchanganyikiwa alipoona kifua cha Chiku, Chiku alikasirika akamsukuma mwalimu mpaka akajigonga kwenye meza ya kioo ambayo ilikuwa nyuma yake na meza ikapasuka, mwalimu Yule alipoteza fahamu palepale, Chiku aliogopa na alilia sana huku anasema, kwa nini mimi kila siku nakua kwenye matatizo, nina kosa gani mimi, nimewakosea nini watu hadi wananisababishia matatizo? Alipoangalia dirishani aliwaona waalimu wanakuja kwa mbali, akajaribu Kufungua madirisha ili aondoke akashindwa, akakumbuka kua funguo zilikua kwenye mfuko wa suruali ya mwalimu, haraka akamsogelea mwalimu na kuchukua funguo, wakati anatoa mkono wake mfukoni akajikata na kipande cha kioo ambacho kilikua kimevunjika kwenye ile meza, ila hakuhisi maumivu, akafungua mlango haraka, ile anatoka nje tu akakutana ana kwa ana na mwalimu mkuu pamoja na waalimu wengine, kwa woga na hofu aliyokua nayo akapata mshtuko mkubwa akadondoka chini  pwaaaa! Kama mzigo palepale akapoteza fahamu, waalimu walishangaa, walopoangalia kwenye ule mlango ambao Chiku ametokea wakaona mtu amelala waliposogea karibu zaidi walishangaa kumuona mwalimu Shebi ameangukia meza na meza imevunjika vunjika, haraka wakapiga simu polisi, polisi wakaja. Wakachunguza eneo la tukio hawakugundua kitu chochote, Chiku na mwalimu Sheby wakawahishwa hospitali. Taarifa zilizagaa kila kona ya jiji kwa muda mchache kwa Kutumia televisheni, redio magazeti na mitandao ya kijamii. Toni na Janeth walipopata taarifa haraka wakaingia kwenye gari lao kuwahi sehemu ya tukio, wakati wapo njiani gari ilikua mwendo kasi sana ili kuwahi eneo la tukio, ghafla gari ikaacha njia na kugonga mti uliopo pembezoni mwa barabara pale pale gari likapinduka juu chini na wote wawili wakapoteza maisha. Waalimu walipata taarifa ya ajali waliyoipata walezi wake Chiku, muda ule ule daktari akatoa taarifa kuwa Chiku ameaga dunia. Lakini mwalimu yupo hai, waalimu walipata pigo kubwa sana kwa kuondokewa na mwanafunzi ambae ndio jicho lao.
            Madaktari walikua makini sana na mgojwa aliyebakia maana wakimpoteza yeye ushahidi wote unaweza ukapotea. Madaktari bingwa wanaotoka hospitali tofauti jijini Dar-es-Salaam waliunganisha ujuzi wao ili kunusuru uhai wa mgojwa Yule, wiki mbili mbele mwalimu Sheby alipata nafuu, waandishi wa Habari hawakucheza mbali kwasababu walikua wanahitaji kumuhoji mwalimu yule. Baada ya afya ya mwalimu yule kukaa vizuri hawakuchelewa wakampeleka kituoni kwa ajili ya mahojiano ya kina juu ya tukio lililotoke, walipojaribu kumuhoji alikana kutoa Ushirikiano na wapelelezi wale, akapelekwa chumba cha adhabu bila kujali kua ametoka hospitali muda mfupi uliopita, baada ya kuona adhabu zimezidi mwalimu Sheby akasema yote yaliyotokea. Hivyo mwalimu sheby alifikishwa mahakamani na hakimu akamuhukumu kifungo cha maisha kwa kosa la kusababisha kifo cha mwanafunzi.
            Waalimu waliwanasihi wanafunzi waliobakia shule waige mfano wa Chiku kwani ni msichana jasiri sana na amekufa kishujaa. Picha za Chiku zilisambaa magazetini na jiji lote lilipata taarifa kuhusu ujasiri wa binti Chiku, Ama kweli kizuri hakidumu.